MAANA YA BARUAPEPE
Baruapepe ni nini
Baruapepe ni ujumbe unaotayarishwa kwa Kutumia tarakirishi na simu janja na kusambazwa kwa njia ya internet.Ujumbe kutoka kwa mtumiaji mmoja wa tarakirishi/simu janja kwenda kwa mpokeaji mmoja au zaidi kupitia mtandao na kujibiwa kwa njia hiyo.

Faida ya kutumia baruapepe
1.Kufanya mawasiliano yasiyo na mipaka kimataifa
2.Kupungua kwa gharama
3.Kushirikishana taarifa
4.Rahisi kurejelea
5.Ni rahisi kutuma
6.Humfikia mlengwa kwa haraka
Athari za matumizi ya baruapepe
1.Uwingi wa taarifa enye kikasha chako bila wewe kupenda
2.Usipokuwa makini unaweza kutuma taarifa kwa asiyehisika
3.Ni rahisi kiambatisho cha baruapepe kusafiri na virusi kutoka sehemu moja kwenda nyingine
4.Baruapepe taka kutoka kwa wadukuzi huweza kuingia bila wewe kuruhusu
Jinsi ya kujisajili kwenye baruapepe
Hatua ya 1
Tembelea anwani ya tovuti'www.gmail.com'na ubonyeze kitufe kilichoandikwa ingia/enter kisha bonyeza walipoandika fungua akaunti/create account.

Hatua ya 2
Baada ya kubonyeza'Fungua akaunti/create account 'jaza taarifa zote zinazotakiwa katika fomu itakayoonekana, baada ya kumaliza kuijaza bonyeza walipoandika endelea/Next.

Hatua ya 3
Hatua hii inakukaribisha kwa utambulisho wa baruapepe uliyoichagua, kisha itakulazimu kujaza namba ya simu yako na utajaza baruapepe ya kurejeshea akaunti yako endapo utakuwa umesahau nywila.

Hatua ya 4
Thibitisha namba yako ya simu.Ili kuthibitisha utspokea ujumbe mfupi wenye matini unayotakiwa kuijaza katika kisanduku kama inavyoonekana kwenye simu. Mfano G-126645

Hatua ya 5
Hatua hii itakufikisha kwenye dirisha lenye mwonekano wa akaunti yako ya baruapepe iliyosajiliwa teyari kwa matumizi.

Hatua ya 6
Unaweza kusoma ujumbe uliotumwa kwenye kikasha cha baruapepe. Bonyeza kichwa cha habari cha ujumbe ambao utafunguka kwa ajili ya kusoma

0 Comments: