*📢 TAARIFA MUHIMU KWA WAKUU WA SHULE NA WATAKWIMU WOTE NCHINI 📚💻*
Kwenye Mfumo wa SIS – Wakati wa Data Cleaning Ukiendelea
*UWEPO WA VITABU SHULENI*
Ndugu Wakuu wa Shule na Watakwimu,
Mnapaswa kuhakiki taarifa za vitabu vilivyopo shuleni kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha taarifa zinazowekwa kwenye mfumo wa SIS ni sahihi na zinaendana na uhalisia wa shule husika. ✅
Hii inasaidia serikali kupitia wizara ya Elimu kujua mahitaji ya vitabu Kwa kila shule na Kuwasambazia.
*Inasaidia Kujua Uwiano Wa wanafunzi katika Shule Na vitabu Vilivyopo Kwa kila somo.*
📚 Vitabu vinavyopaswa kuhakikiwa ni pamoja na:
🔹 Text Books (Kufundishia Kutoka tie)
🔹 Syllabus
🔹 Kiongozi cha Mwalimu
🔹 Vitabu vingine vya kujifunzia na kufundishia for Reference
🖥️ Hatua za kufanya kwenye Mfumo wa SIS
*In short*
➡️ Ingia kwenye menu ya Inventory
➡️ Kisha chagua Books Tracking
Pale Ndio Utaweza ongeza vitabu na pia Kupunguza vitabu.
✍️ Hapo unatakiwa kuingiza taarifa za vitabu mlivyopokea kwa kila somo na darasa husika.
*⚠️ Muhimu Kufahamu:*
Mfumo wa SIS unaruhusu kufanya editing ya taarifa za vitabu ambazo ziliingizwa kimakosa.
*📌 Mfano:*
Shule inaweza kuwa iliingiza vitabu vya somo fulani kwa darasa moja kwa idadi kubwa kuliko hata jumla ya wanafunzi waliopo shuleni. Hivyo ni muhimu kufanya uhakiki na marekebisho mapema.
📌 Pia, kuna baadhi ya shule hazijaingiza hata kitabu kimoja kwenye mfumo, wakati vitabu hivyo tayari wamevipokea kutoka Halmashauri zao. Hali hii inapaswa kurekebishwa haraka.
*🎯 Hivyo basi,*
Tunawasihi Wakuu wa Shule na Watakwimu wote kuhakikisha taarifa za vitabu zinaingizwa kwa usahihi na kuhakikiwa mapema ili kurahisisha zoezi la Data Cleaning na kuboresha ubora wa taarifa kwenye mfumo wa SIS. ✅
🙏 Ushirikiano wenu ni muhimu sana katika kuhakikisha mfumo unakuwa na taarifa sahihi na zenye tija.
Sharing is Caring please share it with your organisation
Follow channel Hii Kwa Mafunzo ya Kitehema Mashuleni.
https://whatsapp.com/channel/0029VaEmbFZ1Hsq6oycc992g
Imeandaliwa na
Mwalimu Na Mifumo
📞 0753538043
TAZAMA HAPA HATUA ZOTE



