Thursday, August 14, 2025

JINSI MKUU WA KITUO UNAVYOWEZA KUWAPA MARKS WATU WAKO UNAOWASIMAMIA USIJE WAPONZA WAKAONEKANA HAWAJAFANYA KITU.

MKUU WA KITUO WAPE MARKS WATU WAKO UNAOWASIMAMIA USIJE WAPONZA WAKAONEKANA HAWAJAFANYA KITU.

Tazama hapa Jinsi ya Kumpa marks Mtu wako wa Chini๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

PEPMIS MODULE YA UPIMAJI (ASSESSMENT)
Jinsi ya Kuweka scores/marks 

Tazama/soma hapa jinsi gani mkuu WA kituo anaweza wawekea watu wake WA chini marks.

Step zipo saba kama picha inavyoonesha hapo juu.

1. Ukisha ingia kwenye menu ya PEPMIS Kisha Bonyeza kipengere kidogo Cha Employee Performance assessment  kipo upande WA kushoto chini namba moja kwenye picha baada ya hapo
2. BONYEZA kwenye menu ya employees Assessment kwenye picha hapo juu ni namba 2
3. Itajitokeza list ya watu wako unaowasimamia kama picha Namba tatu inavyoonesha Kisha katika hiyo list utabonyeza jina la Mtumishi unayetaka kumpa marks, ukisha BONYEZA jina lake
4. Zitajitokeza sub-task zake zote ambazo amefanyia implementation. Unachotakiwa kukifanya sasa ni 
5. BONYEZA kwenye neno asses upande WA kulia juu. Kwenye picha hapo ni namba 4  Pana kinyundo kipo hapo. Bofya hapo. Kisha 
6. Baada ya KUBONYEZA kwenye menu ndogo ya asses kule juu zitakuja sub-task zake Tena kama namba 5 kwenye picha  navyoonesha. Baada ya hapo BONYEZA task unayotaka kumpa/kumwongezea alama 
7. Then itajitokeza menu ndogo yenye ile task ulioichagua yenye qualitative na quantitative . 
8. BONYEZA dot tatu mbele ya qualitative Kisha BONYEZA neno asses qualitative.
Hapo sasa itakupa uwanja WA kuingiza marks.
Published from Blogger Prime Android App

Sasa ni jinsi gani unaingiza hizo marks 

1. Kwa task ambayo ipo completely unaweza unaweza marks 0-100 ni wewe tu kuona kile ameandika kukifanya je kakifanyia kazi kweli Kwa ufanisi?? Au kafanya ilimradi so ni uwanja wako wewe kuandika marks unayoona ni sahihi Kwa namna amefanya Ile kazi.
2. Kwa sub-task ambayo Ipo InProgress hapa unaangalia kama progress ya task ameshaifanya Kwa asilimia ngapi. Je ipo juu ya hamsini au bado hajafikisha hamsini. Kwa maana marks utakayo itoa pale utaitoa kutokana na kazi ambayo tayari kasha ifanya huku ukijua kuwa bado hajaikamilisha .

Kwa Kumaanisha kuwa
Kwa kazi ambayo ipo InProgress score utakuwa unaingiza Kila mara mtumishi atakapo implementation tena kazi yake kule kwenye implementation

Mfano kama mwanzo ulimwekea score 30 then akaja akafanyia implementation tena unafanya assessment Tena unaangalia je unamwongezea marks ngapi kwenye Ile 30 ya mwanzo, Kwa maana unaweza ongeza kutoka 30 mpaka 40+ 

So, utafanya hivyo mpaka sub-task yake itakapo kuwa completed.

*UFAFANUZI KWA WAKUU WA VITUO NA WASIMAMIZI WA WATUMISHI – KUHUSU MUDA SAHIHI WA ASSESSMENT*

*๐Ÿ“Œ Tunapenda kutoa msisitizo huu muhimu kwa Maafisa wote wanaosimamia watumishi kazini, hasa katika kipindi cha mwaka wa kalenda (Calendar Year):*


*⚠️ Tatizo Lililopo:*

Licha ya kuwepo kwa *maelekezo na miongozo rasmi*, bado baadhi ya wakuu wa vituo wanafanya *assessment za kazi (task)* wakati hazijakamilika (*on progress*), 

jambo ambalo linapingana na msingi mzima wa tathmini yenye tija.


*๐Ÿ“š Mfano wa Kuonyesha Upungufu wa Utaratibu Huu:*

Ni sawa na mwanafunzi kufanya swali moja pekee kwenye mtihani, halafu akaomba asahishiwe swali hilo na apewe alama. 

Kisha baada ya muda mfupi afanye swali lingine, nalo  akaomba tena asahishiwe mara moja.

*Hili ni kosa la kimfumo, na linaharibu  ubora wa tathmini.*


*✅ Msingi Sahihi wa Assessment:*

1. *Assessment ifanyike kwa task zilizofikia 100% completion*  

   ♻️ Hii huonyesha kuwa kazi imekamilika, matokeo yake yanaonekana na tathmini inaweza kufanyika kwa haki.

2. *Assessment ifanyike mwisho wa mwaka (Mwezi wa 12)*  

   ♻️Huu ndio muda wa kufanya *Annual Performance Review* kwa mujibu wa mfumo wa utumishi wa umma.

3. *Isipokuwa kwa mazingira maalum kama:*

   ♻️ Mtumishi *anahama kituo cha kazi*

   ♻️Mtumishi *amepewa majukumu mengine na kuachana na yaliyopita*

Katika hali hizo, assessment ya task iliyopo inaweza kufanyika mapema kabla ya mabadiliko hayo kutekelezwa.


*๐Ÿ” Tuweni na Subira na Nidhamu ya Mfumo*

Tusikimbilie kufanya assessment kwa kazi ambazo bado zipo hatua ya utekelezaji, kwa kuwa:

- Zinatoa picha isiyo sahihi ya utendaji
- Zinaleta usumbufu wa kurekebisha makosa baadaye
- Zinavuruga mchakato wa tathmini wa mwisho wa mwaka


*๐Ÿ‘ฅ Wito kwa Ma-Supervisor:*

Simamia kwa weledi. Waelimishe watumishi wako juu ya hili.  

*Assessment si kazi ya muda wote – ni zoezi mahsusi lenye muda wake.*

Tusimame pamoja kuhakikisha tathmini za mwaka zinafanyika kwa haki, kwa ufanisi, na kwa wakati unaostahili.

Kila shule inapendekezwa *kutenga muda maalum kila wiki* (kwa mfano mara 1 au 2) kwa walimu *kukutana na kushirikiana ujuzi wa TEHAMA*. Hili sio hiari, ni *agizo rasmi la serikali* na linaenda sambamba na utekelezaji wa mtaala mpya.


๐ŸŽฅ MAFUNZO HAYA PIA YANAPATIKANA KWA NJIA YA MTANDAONI

Ili kuendelea kujifunza, fuatilia *mafunzo ya kipengele kwa kipengele* kupitia majukwaa yafuatayo ya *ElimikaLeo*:

๐Ÿ“ฒ *WhatsApp Channel:*  

๐Ÿ“˜ *Facebook:*  

By 
ElimikaLeo
 

0 Comments:

Advertisement