Monday, July 20, 2026

Mabadiliko mapya ya kazimradi(Project) katika somo la Business studies

*NECTA NECT NECTA NECTA NECTA NECTA NECTA*

*๐Ÿ“ข HII NI KUTOKA NECTA MABADILIKO MAPYA YA KAZIMRADI (PROJECTS) KATIKA SOMO LA BUSINESS STUDIES*

Habari za majukumu wanachama wa chaneli hii!
Leo tunaleta uchambuzi wa kina kuhusu mwongozo mpya wa Kazimradi (Project-Based Assessment - PBA) katika somo la *Business Studies* kutoka Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA).

Lengo ni kuhakikisha kila mdau anafahamu wajibu wake, hatua za utekelezaji, pamoja na ratiba rasmi ili utekelezaji wa miradi hii uwe wenye mafanikio.


*๐ŸŽฏ LENGO KUU LA KAZIMRADI (PROJECTS)*

Kazimradi hizi zimeandaliwa na NECTA na kuwekwa kwenye tovuti yao pamoja na mfumo wa PReMS kwa wanafunzi wa:

✅ Kidato cha Kwanza
✅ Kidato cha Pili
✅ Kidato cha Tatu

Malengo ya Kazimradi:
๐Ÿ”ฅ Kumsaidia mwanafunzi kutumia maarifa ya biashara kutatua changamoto halisi za jamii.

๐Ÿ”ฅ Kukuza stadi za vitendo, ubunifu, ushirikiano, ujasiriamali, na fikra kinzani.

๐Ÿ”ฅ Kujenga uzalendo na uwajibikaji unaoendana na dira ya taifa ya maendeleo ya viwanda na kujiajiri.

*๐Ÿ“Š MCHANGO WA ALAMA KWENYE MATOKEO YA MWISHO*

๐Ÿ“Œ Kazimradi hizi ni endelevu na zitafanyika kila muhula.

๐Ÿ“Œ Kazimradi ya Kidato cha Tatu Muhula wa Pili itakamilishwa mwanafunzi anapoingia Kidato cha Nne Muhula wa Kwanza.

๐Ÿ“Œ Katika somo la Business Studies, kazimradi itachangia jumla ya alama 7 katika Alama Endelevu (C.A) za mwanafunzi zitakazotumika kuchakata matokeo ya mwisho.

๐Ÿ“Œ Alama hizi ni mahsusi kwa somo la Business Studies pekee.


*๐Ÿ› ️ MIONGOZO RASMI ILIYOTOLEWA NA NECTA*

NECTA imeandaa nyaraka mbili muhimu kwa ajili ya utekelezaji wa PBA:

๐Ÿ“˜ Project Based Guidelines
๐Ÿ“— Project Based Implementation Manual

*Nyaraka hizi zinapatikana kupitia tovuti ya NECTA pamoja na mfumo wa PReMS.*

*๐Ÿ‘ฅ WAJIBU WA WADAU MBALIMBALI*

⚡ 1. Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA)
๐Ÿ”น Kuratibu utekelezaji wa PBA kitaifa.
๐Ÿ”น Kusambaza miongozo rasmi ya miradi.
๐Ÿ”น Kuhakikisha miradi inaendana na mtaala na matokeo ya ujifunzaji.
๐Ÿ”น Kusimamia ukusanyaji, uhakiki, na utunzaji wa alama zote.

⚡ 2. Wakuu wa Shule*
๐Ÿ”น Kusimamia utekelezaji wa PBA ngazi ya shule.
๐Ÿ”น Kutoa msaada kwa walimu na kuhakikisha usahihi wa alama.
๐Ÿ”น Kuwasilisha matokeo yaliyohakikiwa kupitia mfumo wa PReMS.

⚡ 3. Walimu wa Taaluma*
๐Ÿ”น Kusimamia utekelezaji wa miradi kwa kuzingatia mtaala.
๐Ÿ”น Kutoa mwongozo kwa walimu wa somo.
๐Ÿ”น Kuhakikisha tathmini inafanyika kwa haki na usawa.

⚡ 4. Walimu wa Somo la Business Studies*
๐Ÿ”น Kutambulisha malengo, ratiba, na mahitaji ya miradi mwanzoni mwa muhula.
๐Ÿ”น Kusimamia na kufuatilia maendeleo ya wanafunzi kwa kutumia fomu maalumu.
๐Ÿ”น Kufanya tathmini kwa kutumia vigezo sanifu (rubrics) vya NECTA.
๐Ÿ”น Kukusanya na kuwasilisha alama kwa Mkuu wa Shule.

⚡ 5. Wanafunzi*
๐Ÿ”น Kushiriki kikamilifu katika kazi za vikundi.
๐Ÿ”น Kutumia maarifa ya biashara kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi.
๐Ÿ”น Kuandaa na kuwasilisha miradi kwa njia ya:

- Ripoti za maandishi
- Mabango (posters)
- Mifumo ya kidijitali

*⏱️ MCHAKATO WA UTEKELEZAJI*

๐Ÿš€ Kazi za miradi zitafanyika kwa kipindi cha wiki 6 hadi 8.

๐Ÿš€ Wanafunzi watakusanya taarifa, kufanya mahojiano, na kushirikiana katika vikundi.

๐Ÿš€ Miradi itawasilishwa mbele ya jopo la walimu na wadau husika kwa kutumia:
- Mabango
- Vielelezo (models)
- Ripoti

๐Ÿš€ Vigezo vya utoaji wa alama vitazingatia:
✅ Ubunifu
✅ Usahihi
✅ Mpangilio
✅ Mawasiliano
✅ Matumizi ya dhana za somo

*♿ USHIRIKISHWAJI WA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM*

Shule zinapaswa kuhakikisha usawa kwa:
✔ Kubadilisha majukumu ya miradi kulingana na aina ya ulemavu.
✔ Kutoa vifaa saidizi kama Braille au wakalimani.
✔ Kuruhusu muda wa ziada pale inapobidi.
✔ Kuwashirikisha walimu wa elimu maalum katika usimamizi.

*๐Ÿ“… KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI – MWAKA 2026*

๐Ÿ“˜ Kidato cha I, II & III (Muhula wa Kwanza)

๐Ÿ—“️ Kutoa Kazimradi:
*09/03/2026 – 20/03/2026*

๐Ÿ—“️ Utekelezaji:
*30/03/2026 – 05/04/2026*

๐Ÿ—“️ Uwasilishaji:
*20/04/2026 – 30/04/2026*

๐Ÿ—“️ Kupandisha Alama (PReMS):
*11/05/2026 – 29/05/2026*

๐Ÿ“˜ Kidato cha I & II (Muhula wa Pili)

๐Ÿ—“️ Kutoa Kazimradi:
*17/08/2026 – 28/08/2026*

*๐Ÿ—“️ Utekelezaji:*
07/09/2026 – 11/09/2026
(Kidato cha II hadi 09/09/2026)

*๐Ÿ—“️ Uwasilishaji:*
28/09/2026 – 11/10/2026

๐Ÿ—“️ Kupandisha Alama (PReMS):
14/10/2026 – 06/11/2026

*๐Ÿ“˜ Kidato cha III (Muhula wa Pili)*

๐Ÿ—“️ Kutoa Kazimradi:
09/03/2026 – 20/03/2026

*๐Ÿ—“️ Utekelezaji:*
07/09/2026 – 09/09/2026

*๐Ÿ—“️ Uwasilishaji:*
28/09/2026 – 11/10/2026

*๐Ÿ—“️ Kupandisha Alama (PReMS):*
14/10/2026 – 06/11/2026

*๐Ÿ“ˆ HALI YA UPAKUAJI WA NYARAKA*

(Takwimu hadi 10/02/2026)

NECTA imebainisha kuwa kasi ya upakuaji wa nyaraka bado ni ndogo. Shule zinahimizwa kuchangamkia fursa hii mapema.

Mpaka mwezi Huu WA Tano 2026
๐Ÿ“Š Shule zilizopakua miongozo (Guidelines & Manual):
2,230 tu (29.71%) kati ya shule 7,506.

๐Ÿ“Š Shule zilizopakua Kazimradi (Projects):
1,332 tu (17.75%) kati ya shule 7,506.

๐Ÿ“Š Shule zilizowasilisha alama za C.A kwenye mfumo wa PReMS:
355 tu (4.73%) kati ya shule 7,506.

*๐Ÿ’ก HITIMISHO*

Ufanisi wa utekelezaji wa Kazimradi hizi unategemea ushirikiano wa karibu kati ya:

๐Ÿค Uongozi wa Shule
๐Ÿค Walimu
๐Ÿค Wanafunzi

Kila mdau anahimizwa kupitia miongozo hii kikamilifu kupitia tovuti ya NECTA ili kuhakikisha uadilifu, usawa, na mafanikio katika tathmini hii ya vitendo.

๐Ÿ“ข Sharing is Caring!
Tafadhali sambaza ujumbe huu kwa walimu na wadau wengine wa elimu ili sote twende sawa.

Imeandaliwa na 
                              Mwalimu na Mifumo*
                               ๐Ÿ“ž 0753 538 043
   

Testme ni mwalimu wa shule ya Awali na Msingi na mwandishi wa maudhui ya elimu nchini Tanzania. Kupitia blog ya MsomiHuru Na Mitihani Tz, anashiriki mitihani, vitabu, andalio la somo, na nyenzo mbalimbali za kujifunzia kwa wanafunzi na walimu.

0 Comments: