Friday, October 25, 2024

JINSI YA KUANDIKA RIPOTI

 Ripoti ya kawaida

Muundo wa ripoti ya kawaida

Ripoti ya kawaida sharti iwe na sehemu kuu nne; sehemu hizo ni:

1. Kichwa cha ripoti
  • Ripoti lazima iwe na kichwa cha habari; kichwa hicho huandikwa kwa maelezo machache, kwa herufi kubwa na kupigwa mstari.
  • Kichwa huoana na yanayoshughulikiwa. Kwa mfano: RIPOTI YA AJALI MBAYA YA GARIMOSHI
2. Utangulizi wa ripoti
  • Utangulizi wa ripoti hueleza kwa muhtasari lengo la ripoti kama ni kutoa taarifa au kumbukumbu.
3. Kiini cha ripoti/mwili
  • Kiini cha ripoti kina maelezo yote kuhusiana na tukio lenyewe; sehemu hii huelezea kwa ufasaha mambo yaliyotokea, chanzo chake, ukubwa wake, wahusika, na tukio linalohusika.
  • Ufafanuzi huu uwe ni wa ukweli wa kuaminika(si lazima iwe tukio la kweli lakini haistahili kumingisha mtu dhana ya uongo).
  • wakati uliopita nanafsi ya tatu hutumika isipokuwa unavyomnukuu myu moja kwa moja.
4. Mwisho wa ripoti
  • Hii ni sehemu ya mwisho ya ripoti. Sehemu hii huonyesha mambo makuu mawili:
  1. maoni/mapendekezo ya mwandishi wa ripoti.
  2. Lazima sentensi "Ripoti hii imeandaliwa na kuandikwa na:" iwe katika hitimisho, kisha kufuatwa na jina na cheo cha mwandishi pamoja

0 Comments:

Advertisement