
Maana ya sayansi
Sayansi ni maarifa yanayopatikana kwa kufanya uchunguzi na majaribio.majaribio kama upimaji wa vitu na uchunguzi kama kutokea kwa Radi.MATAWI YA SAYANSI
Sayansi ina matawi mbalimbali ambapo kila tawi linahusika na aina fulani ya maarifa. Matawi hayo ni kama vile(i)BIOLOGIA
Ni tawi la sayansi linalohusika na viumbehai yaani mimea (Miti) na wanyama (binadamu)(ii) FIZIKIA
Ni tawi la sayansi linalohusika na uhusiano wa maada na nishati. Aina za nishati ni pamoja na joto, mwanga na Umeme(iii) KEMIA
Ni tawi la sayansi linalohusika na muundo na tabia za maada.pia inahusisha mabadiliko yanayotokea katika maada.Kuna hali mbalimbali za maada ikiwemo yabisi(jiwe), Kimiminika(maji) na gesi(hewa na gesi ya oksijeni)TAALUMA ZINAZOHUSIANA NA SAYANSI
Zipo taaluma mbalimbali zinazotokana na kujifunza sayansi, taaluma hizo ni kama vile(i) Udaktari wa binadamu
(ii) Ualimu
(iii) Ufamasia
(iv) Uhandisi
(v) utaalamu wa Kemia
(vi) utaalamu wa mimea
(vii) daktari wa wanyama
UMUHIMU WA SAYANSI
Umuhimu wa sayansi katika maisha ya kila siku(i) Husaidia kujenga maarifa na stadi mbalimbali mfano: ubunifu,udadisi na fikra yakinifu
(ii) kutengeneza vitu na vifaa vinavyotumika nyumbani kama vile sabuni,dawa ya kusafishia meno, vyombo vya chakula
(iii) kutengeneza vitu vinavyotumika mashuleni kama vile chaki,daftari,kalamu na vitabu
(iv) kutengeneza vifaa vya ujenzi Kama saruji,chuma, chokaa,mabati,mabomba na marumaru
(v) kutengeneza vifaa vya kufanyia uchunguzi na utambuzi wa magonjwa na tiba (hadubini)
(vi) kutengeneza vifaa vya kurahisisha mawasiliano mfano:simu,redio na tarakirishi (๐ฅ️ kompyuta)
0 Comments: