Tuesday, July 29, 2025

jinsi ya kutumia ngeli za nomino katika lugha ya kiswahili

 NGELI ZA NOMINO

NGELI ZA NOMINO:Ni makundi ya kisarufi ya majina katika lugha ya kiswahili na baadhi ya lugha za kibantu.Kwa maneno mengine, ngeli za nomino ni utaratibu unaotumika kuweka nomino katika makundi yanayofanana kwa kuzingatia umoja na uwingi wa maneno hayo.silabi zilizokolezwa wino ndio zinazounda aina ya ngeli.

 

Ngeli hizo zipo za namna tisa ambazo zimeainishwa kama ifuatavyo:

 


1.Ngeli ya A-WA

Ngeli hii inahusisha majina ya viumbe hai kama vile watu,wanyama,ndege,wadudu nk.

Umoja                                                                   uwingi

Mfano:Msafiri anakaribia kufika.  Wasafiri wanakaribia kufika

 

2.Ngeli ya U-I

Ngeli hii inahusisha majina ya vitu visivyohai vinavyoanza na sauti M (umoja)na ya(uwingi) pia baadhi ya viungo vya mwili huingia hapa mfano mguu,mkono,mkia nk.

Umoja                                          uwingi

Mfano:Mtiunaungua moto        Miti inaungua moto

 

3.Ngeli ya LI-YA

Ngeli hii hujumuisha majina yenye kiambishi awali(umoja)na ya (uwingi)

Umoja                                                               uwingi

Mfano:Chungwa limeiva.        Machungwa yameiva

 

4.Ngeli ya KI-VI

Hii ni ngeli ambayo hujumuisha majina yanayoanza na ki au ch(umoja) na vi au vy(uwingi)

 

Umoja                                           uwingi

Mfano:Kitandakimetandikwa Vitanda vimetandikwa

Chakulakitaliwa                         Vyakula vitaliwa

 

5.Ngeli ya U-ZI

Ngeli hii hurejelea majina ambayo huanza na U katika umoja na kuchukua ZI kiambishi kiwakilishi cha ngeli katika uwingi.

 

Umoja                                                               uwingi

Mfano:Ufaumejitokeza                                                  Nyufa zimejitokeza

            Ukuta umejengwa                                                Kuta zimejengwa

            Wimbo unachezeka                                             Nyimbo zinachezeka

 

6.Ngeli ya I-ZI

Ngeli hii hutumika kwa majina yasiyobadilika katika umoja wala katika uwingi lakini huchukua viambishi viwakilishi tofauti: i (umoja) na zi (uwingi)

Umoja                                                               uwingi

Mfano:Nyumba imebomoka                            Nyumba zimebomoka

 

7.Ngeli ya U-YA

Ngeli hii hujumuisha nomino zenye kiambishi awali U(umoja) na ma(uwingi)

 

Umoja                                                               uwingi

Mfano:Unyoya unapepea                         Manyoya yanapepea  

 

8.Ngeli ya KU

Katika ngeli hii yanaingia majina yote yanayotokana na kunominisha vitenzi

 

Mfano:Kuimba kumemtajirisha

Kutembea kumemchosha

9.Ngeli ya PAMUKU

Ngeli hii huonesha mahali

Mfano: Hapa petu pazuri                Mfano:  Kule kulikoungua shoka

Mfano: Pale palipo na upendo        Mfano: Mule mulimoungua


 

 

0 Comments:

Advertisement