Saturday, October 04, 2025

JINSI YA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA PSSSF – HIFADHI YA JAMII*

 



MFUKO KWA WATUMISHI.


FUATILIA MICHANGO YAKO KABLA HUJASTAFF.


PATA MAFAO MBALIMBALI.


*📘 JINSI YA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA PSSSF – HIFADHI YA JAMII*


Mfumo wa *PSSSF Member Portal* umetengenezwa ili kuwasaidia watumishi wa umma kuweza kudhibiti na kufuatilia michango yao ya hifadhi ya jamii kwa njia ya kidijitali. Kwa kupitia mfumo huu, mtumishi anaweza:


*🔍 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA KUPITIA PSSSF PORTAL:*

1. *Kuangalia mchango wako wa kila mwezi* – fedha unayokatwa kupitia mshahara wako pamoja na mchango wa mwajiri.

2. *Kusajili au kubadilisha wategemezi wako* (beneficiaries).

3. *Kuomba mafao mbalimbali* kama mchangiaji – mfano: *fao la uzazi*, n.k.



*🖥️ HATUA ZA KUJISAJILI ONLINE (NJIA YA KWANZA)*


👉 Bofya hapa kuanza usajili:  

*https://memberportal.psssf.go.tz/steponeregister*


Kisha fuata hatua hizi:


1. *Chagua "Member"* kwenye sehemu ya kwanza.

2. *Weka Namba yako ya NIDA* kwa usahihi.

3. *Chagua tarehe ya kuzaliwa* (siku, mwezi, mwaka) kama ilivyo kwenye NIDA.

4. *Tengeneza Password Mpya* utakayotumia kila mara kuingia kwenye mfumo huu.

5. *Rudia Password hiyo hiyo* ili kuithibitisha.

6. Bonyeza *Register*.


✔️ Utaambiwa uingize *Confirmation Code* itakayotumwa kwenye namba yako ya simu. Hakikisha simu ipo mkononi wakati wa usajili.


✔️ Baada ya kuthibitisha, utapewa nafasi ya *ku-login*, na hapo utakuwa umekamilisha usajili.



*📲 NJIA YA PILI – KUPITIA APP YA PSSSF*


Kama njia ya kwanza haitafanikiwa:

1. Ingia *Play Store*.

2. *Download App ya "PSSSF Member Portal"*.

3. Fanya usajili kama ilivyoelekezwa hapo juu kupitia app.



*📢 KWA MSAADA NA ELIMU ZAIDI Follow Channel Hii Na share Kwa Staffmate wako*


📲 WhatsApp Channel:  

https://whatsapp.com/channel/0029Vb2b7U5CBtxLx6kwOb1m


📘 Facebook:  


https://www.facebook.com/profile.php?id=61574011348247


*By:*  

*ElimikaLeo*

Testme ni mwalimu wa shule ya Awali na Msingi na mwandishi wa maudhui ya elimu nchini Tanzania. Kupitia blog ya MsomiHuru Na Mitihani Tz, anashiriki mitihani, vitabu, andalio la somo, na nyenzo mbalimbali za kujifunzia kwa wanafunzi na walimu.

0 Comments: