Oct 4, 2025

JINSI YA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA PSSSF – HIFADHI YA JAMII*

 



MFUKO KWA WATUMISHI.


FUATILIA MICHANGO YAKO KABLA HUJASTAFF.


PATA MAFAO MBALIMBALI.


*📘 JINSI YA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA PSSSF – HIFADHI YA JAMII*


Mfumo wa *PSSSF Member Portal* umetengenezwa ili kuwasaidia watumishi wa umma kuweza kudhibiti na kufuatilia michango yao ya hifadhi ya jamii kwa njia ya kidijitali. Kwa kupitia mfumo huu, mtumishi anaweza:


*🔍 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA KUPITIA PSSSF PORTAL:*

1. *Kuangalia mchango wako wa kila mwezi* – fedha unayokatwa kupitia mshahara wako pamoja na mchango wa mwajiri.

2. *Kusajili au kubadilisha wategemezi wako* (beneficiaries).

3. *Kuomba mafao mbalimbali* kama mchangiaji – mfano: *fao la uzazi*, n.k.



*🖥️ HATUA ZA KUJISAJILI ONLINE (NJIA YA KWANZA)*


👉 Bofya hapa kuanza usajili:  

*https://memberportal.psssf.go.tz/steponeregister*


Kisha fuata hatua hizi:


1. *Chagua "Member"* kwenye sehemu ya kwanza.

2. *Weka Namba yako ya NIDA* kwa usahihi.

3. *Chagua tarehe ya kuzaliwa* (siku, mwezi, mwaka) kama ilivyo kwenye NIDA.

4. *Tengeneza Password Mpya* utakayotumia kila mara kuingia kwenye mfumo huu.

5. *Rudia Password hiyo hiyo* ili kuithibitisha.

6. Bonyeza *Register*.


✔️ Utaambiwa uingize *Confirmation Code* itakayotumwa kwenye namba yako ya simu. Hakikisha simu ipo mkononi wakati wa usajili.


✔️ Baada ya kuthibitisha, utapewa nafasi ya *ku-login*, na hapo utakuwa umekamilisha usajili.



*📲 NJIA YA PILI – KUPITIA APP YA PSSSF*


Kama njia ya kwanza haitafanikiwa:

1. Ingia *Play Store*.

2. *Download App ya "PSSSF Member Portal"*.

3. Fanya usajili kama ilivyoelekezwa hapo juu kupitia app.



*📢 KWA MSAADA NA ELIMU ZAIDI Follow Channel Hii Na share Kwa Staffmate wako*


📲 WhatsApp Channel:  

https://whatsapp.com/channel/0029Vb2b7U5CBtxLx6kwOb1m


📘 Facebook:  


https://www.facebook.com/profile.php?id=61574011348247


*By:*  

*ElimikaLeo*

0 Comments: