HALMASHAURI YA WILAYA YA _________, SHULE YA MSINGI _________MTIHANI WA UPIMAJI, DARASA LA IVSOMO : KISWAHILIMuda : saa 1:40 ___________ ____ 2025
SEHEMU A (Alama 20)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Sikiliza kwa makini sentensi zifuatazo kisha uziandike kwa usahihi katika nafasi
zilizoachwa wazi.
(i)_________________________________________________
(ii) _________________________________________________
(iii) _________________________________________________
(iv) _________________________________________________
(v)_________________________________________________
2. Katika kipengele cha (i) - (x), chagua jibu sahihi, kisha andika herufi yake katika kisanduku
ulichopewa.
(i) Gari hii ni ya kifahari kwa sababu inauzwa kwa .............................. kubwa
A Samani B. Zamani C. Thamani D. Dhamani ( )
(ii)Mtoto mzuri ni yule mwenye adabu kwa watu. Kisawe cha nenolililopigiwa mstari ni kipi?
A heshima B. Akili C. utundu D. uvivu ( )
(iii) Mjomba wangu anafanya kazi ya kuendesha mabasi ya wanafunzi. Je, mjomba wangu ni nani?
A. mwalimu B. rubani C. mwanafunzi D. dereva ( )
(iv) ni mazungumzo amabayo hufanywa na watu Zaidi ya wawili kuhusu mada Fulani ili kujenga
hoja na mawazo katika mada iliyoandaliwa na mwisho kupata mwafaka wa wa jambo
linalozungumziwa A. mjadala B .risala C. barua D. nyimbo ( )
(v) usemi wa kisanii wa kimapokeo unaofikiriwa na jamii kuwa kweli na unaotumiwa kufumbia au
kupigia mfano na huwa umebeba maana pana kuliko maneno yenyewe yanayotumiwa
A. methali B. vitendawili C. nahau D. hadithi ( )
(vi) Ni kauli zilizojengwa kwa picha kwa kutumia maneno ya kawaida lakini zikatoa maana isiyo ya
kawaida A. Nahau B. Methali C. Misemo D. vitendawili ( )
(vii) Mwajuma ni kitinda mimba katika familia ya mzee Ernest neno kitinda mimba linamaana sawa
na neno gani?A.mtoto mwenye akili B.Mtoto wa kwanza C. Mtoto wa mwisho D.
Mtoto mtukutu ( )
(viii) "Aliondoka asubuhi na mapema" sentensi hii ipo katika wakati gani? A. wakati uliopo
B. Wakati uliopita C. Wakati ujao D. Wakati uliopo unaoendelea ( )
(ix) Ili tuweze kufaulu katika masomo yetu________ kusoma kwa bidii
A. Ni budi B.Hatuna budi C. Siyo budi D. Budi ( )
(x)Kinyume cha neno mbivu ni kipi? _____A.Changa B.Chungu C. Mbichi D.Chachu
SEHEMU B (Alama 20)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
3. Soma kwa umakini Nahau, methali na vitendawili zifuatazo kisha Jaza nafasi zilizoachwa wazi
(i)Piga mtu ukope maana yake ni __________________________
(ii)Andika nahau yenye maana hii "TAZAMA" ______________
(iii)Pigwa butwaa maana yake ni _______________________
(iv)Viti vyote nimekalia isipokuwa hicho. ________________
(v)Kamilisha kitendawili hiki: "Popoo mbili zavuka mto _______
4. Umepewa sentensi tano (i) – (v) zilizochanganywa. Panga katika mtiririko unaoleta maana ili kuunda kifungu cha habari kwa kuzipa herufi A, B, C, D na E katika nafasi zilizoachwa wazi.
(i) Natandika kitanda changu vizuri. [ ]
(ii)Kisha nakunywa chai na baadaye naondoka kwenda shule. [ ]
(iii)Halafu naoga na kupiga mswaki vizuri. [ ]
(iv) Kila siku huwa naamka saa kumi na mbili kamili asubuhi [ ]
(v)Ninavaa sare za shule halafu nakwenda kuwasalimu wazazi [ ]
SEHEMU C (Alama 10)
Jibu swali la tano (5).
5. Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali
Kila nikitafakari, namuona wa muhimu
Amejawa kubwa ari, kutupatia elimu
Sikazi ya kifahari, imejaa mashutumu
Bila ya wewe mwalimu, hakuna wa kujivuna
Sote tutoe kongole, kwa kazi yake mwalimu‟
Sisi sote ni zaole, tuache kuwa wagumu
Tumpe kiti cha mbele, kwa heshima ya elimu
Bila wewe mwalimu, hakuna wa kujivuna
MASWALI
i.Shairi ulilosoma lina jumla ya beti ngapi_______________________
ii.Ubeti wa pili una jumla ya mizani ngapi_______________________
iii.Vina vya mwisho katika ubeti wa kwanza ni vipi ________________
iv.Nani ametajwa kuwa ni Msingi wa taaluma zote ________________
v. Funzo gani unapata katika shairi hili__________________________
0 Comments: